UFISADI UMEKITHIRI, RAIS KENYATTA UPO?

Leo mi ni Mwananchi, kesho

huenda nikawa rais, mola niepushe

na ibilisi sije nikawa rahisi

kushindwa kuiongoza nchi na wote

kwangu chini kwa ufisadi kawa

wepesi. Mumba niepushe na swali kama hili; mnataka nifanye nini?

Wangu ndungu wasiwe wenye nchi,

Kunizuia kutimiza yangu ahadi,

wanainchi kuwaibia ni ufisi, kunyamaza kwa rais ni kuunga mkono ufisi,

Baadaye kuwadanganya wako wateuzi kwa maswali,

Jamani mwataka nifanye nini?

Basi swali nalipa jibu,

Kama mwalimu nikutie nithamu

Mwazo rekebibisha makosa aliyeyafanya baba na babu,

Hatujalisahau hilo na basi pia ni muhimu,

Mameno matupu na kufoka ka yule wapili nikufuata nyayo,

Wakenya wabaki masikini na kufanya michezo uga nyayo,

simama wima ufanye vitendo kama Matiangi upunguze mitindo,

Anaye itaji kunyongwa na kaburi lake liwe kama wetu mfano,

Anaitaji kwenda jela basi na nyumbani asahau ndio asikufanye ovyo,

Kama michuki uweke msimamo,

Yafanye hayo na kesho tutakubali utuulize,

Natosha kuwa rais wa Afrika?